DPO SIMAMIA USALAMA WA TAARIFA BINAFSI KWENYE TAASISI/KAMPUNI YAKO
July 9, 2025, 5:26 p.m.
Maafisa ulinzi wa taarifa (DPOs) wametakiwa kuhakikisha wanasimamia ulinzi wa taarifa binafsi kwenye taasisi zao.
Hayo yamesemwa leo Jumatano tarehe 9/7/2025 na Bi. Asha Sinare, mwezeshaji wa mafunzo kwa maafisa ulinzi wa taarifa ikiwa ni siku ya kwanza ya mafunzo maalum ya siku tatu kwa maafisa hao kutoka taasisi za umma na binafsi.
“Afisa Ulinzi wa taarifa binafsi (DPO) unapaswa kuwa na maarifa juu ya usalama wa mtandao ili uelewe hatari zilizopo zinazoathiri ulinzi wa taarifa binafsi kwenye taasisi/kampuni yako. Shughuli zote za kampuni zinazotumia taarifa binafsi za watu, DPO lazima uzitambue na uhakikishe utekelezaji wake unazingatia ulinzi wa faragha za taarifa hizo” amesema Bi. Aisha Sinare
Mafunzo ya maafisa ulinzi wa taarifa ni moja ya njia ya PDPC kuhakikisha maafisa hao wanaelewa na kutekeleza majukumu yao ya ulinzi wa faragha za watu kwenye taarifa binafsi zilizopo kwenye taasisi/kampuni zao.
Ulinzi wa taarifa binafsi ni takwa la kisheria na Tume ya Ulinzi wa taarifa binafsi inalisimamia hilo kuhakikisha utekelezaji wa Sheria ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi, Sura ya 44 unafanyika kikamilifu.

PDPC YASHIRIKI KIKAO - TATHMINI YA…

DKT. MKILIA AFUNGUA WARSHA JUKWAA …

PDPC Yatoa Mafunzo Maalumu kwa Bod…

ELIMU YA DHANA YA ULINZI WA TAARIF…

PDPC YATOA ELIMU KWA UMMA MWANZA

ULINZI WA TAARIFA BINAFSI NI SWALA…

PDPC YATOA WITO WA USAJILI WA TAAS…

MISHAHARA KWA WAFANYAKAZI NCHINI K…

PDPC YATANGAZA MAFUNZO KWA MAAFISA…

SIMAMIENI MIPANGO YA KUPUNGUZA VIH…

RISK CHAMPIONS NA DPO’s SHIRIKIANE…

WARATIBU NA WASIMAMIZI WA VIHATARI…

DPIA NI LAZIMA, KABLA YA KUANZISHA…

RIDHAA INAPASWA KUTOLEWA BILA SHUR…

TANZANIA DELEGATION PARTICIPATES I…

ROPA NI MUHIMU KWA KILA DPO

𝐓𝐀𝐍𝐙𝐀𝐍𝐈𝐀 𝐀𝐓𝐓𝐄𝐍𝐃𝐄𝐃 𝐓𝐇𝐄 𝐖𝐒𝐈𝐒+𝟐𝟎 𝐇𝐈𝐆𝐇…

DPO SIMAMIA USALAMA WA TAARIFA BIN…

NI LAZIMA KUWA NA SERA YA ULINZI W…

DPIA NI MUHIMU KUIMARISHA ULINZI W…