JENGA UAMINIFU WA TAASISI YAKO KWA WADAU KWA KULINDA TAARIFA ZAO BINAFSI
Aug. 20, 2025, 8:57 p.m.
Ikiwa ni siku ya kwanza ya awamu ya nne ya mafunzo maalum kwa Maafisa ulinzi wa Taarifa Binafsi kutoka kwenye taasisi za umma na binafsi nchini, maafisa hao wametakiwa kuhakikisha taarifa binafsi za wadau wa taasisi zao zinalindwa kwa mujibu wa Sheria ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi, Sura ya 44.
Akitoa mafunzo hayo Bi. Hellen Achimpota leo tarehe 20 Agosti, 2025 mkoani Morogoro amesema ni muhimu kuzingatia ukusanyaji wa taarifa binafsi unafanywa kwa lengo maalum tu, na kuhakikisha kuwa taarifa hizo hazitumiki nje ya madhumuni yaliyokusudiwa. Kwa kufanya hivyo taasisi hizo zitakuwa zinazingatia misingi ya kisheria ya faragha na heshima kwa haki za watu binafsi.
"Katika dunia ya sasa inayotawaliwa na teknolojia na matumizi makubwa ya taarifa za watu, ni muhimu kwa maafisa wa ulinzi wa taarifa binafsi kuelewa wajibu wao wa kisheria na kiutumishi. Misingi ya ukusanyaji wa idadi ya taarifa kulingana na makusudi husika , usalama wa taarifa, uhifadhi sahihi na usiri ni nguzo kuu katika kulinda haki ya faragha ya mtu binafsi," alisema Bi. Hellen
Katika mafunzo hayo, washiriki wamepata fursa ya kujadili mifano halisi ya changamoto wanazokutana nazo kazini na kushiriki katika mazoezi kwa vitendo yaliyowasaidia kuweka mikakati madhubuti ya kuimarisha ulinzi wa taarifa binafsi watakaporudi katika taasisi zao.
Mafunzo haya yanatarajiwa kuwa chachu ya maboresho katika usimamizi wa taarifa binafsi ndani ya taasisi mbalimbali, sambamba na utekelezaji wa Sheria ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi nchini.

SIMAMIENI MIPANGO YA KUPUNGUZA VIH…

RISK CHAMPIONS NA DPO’s SHIRIKIANE…

WARATIBU NA WASIMAMIZI WA VIHATARI…

DPIA NI LAZIMA, KABLA YA KUANZISHA…

RIDHAA INAPASWA KUTOLEWA BILA SHUR…

TANZANIA DELEGATION PARTICIPATES I…

ROPA NI MUHIMU KWA KILA DPO

𝐓𝐀𝐍𝐙𝐀𝐍𝐈𝐀 𝐀𝐓𝐓𝐄𝐍𝐃𝐄𝐃 𝐓𝐇𝐄 𝐖𝐒𝐈𝐒+𝟐𝟎 𝐇𝐈𝐆𝐇…

DPO SIMAMIA USALAMA WA TAARIFA BIN…

NI LAZIMA KUWA NA SERA YA ULINZI W…

DPIA NI MUHIMU KUIMARISHA ULINZI W…

PDPC KUANZISHA ITHIBATI KWA MAAFIS…

ELIMU YA DHANA YA ULINZI WA TAARIF…

BALOZI ADADI AONGOZA KIKAO CHA BOD…

JENGA UAMINIFU WA TAASISI YAKO KWA…

NI KOSA KUSAMBAZA TAARIFA ZA MTU K…

𝐊𝐔𝐀𝐍𝐃𝐀𝐀 𝐒𝐄𝐑𝐀 𝐘𝐀 𝐔𝐋𝐈𝐍𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐓𝐀𝐀𝐑𝐈𝐅𝐀 …

𝐔𝐒𝐈𝐖𝐄𝐊𝐄 𝐓𝐀𝐀𝐑𝐈𝐅𝐀 𝐙𝐀 𝐌𝐓𝐔 𝐊𝐀𝐌𝐀 𝐌𝐃𝐇𝐀𝐌𝐈…

KUSAFIRISHA TAARIFA BINAFSI NJE YA…
.
