KAMPENI ZIZINGATIE ULINZI WA FARAGHA KWENYE TAARIFA BINAFSI ZA WATU
Sept. 5, 2025, 8:53 a.m.
Mkurugenzi Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi Ofisi ya Zanzibar, Bi Rehema Abdalla amewataka wagombea wa ngazi zote nchini kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 kuhakikisha hawaingilii faragha za watu.
Bi. Rehema amezungumza hayo wakati akifanya mahojiano maalum na mtangazaji Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) Bi. Nasra Khatib kuhusu umuhimu wa kulinda taarifa binafsi katika kampeni za uchaguzi mkuu kwa wagombea watakaonadi sera za vyama vyao.
“Wagombea wa ngazi zote hakikisheni hamuingilii faragha za watu na majukwaa mnayotumia kunadi sera za vyama vyenu yasitumike kukiuka misingi ya Sheria ya Ulinzi wa taarifa binafsi” amesema Bi. Rehema.
Akisisitiza swala hili, Bi. Rehema amesema kuwa kuchapisha taarifa binafsi za mtu kwenye magazeti, mitandao ya kijamii au kutangaza kwenye redio na televisheni bila ridhaa ya muhusika wa taarifa hizo ni kinyume na matakwa ya Sheria ya Ulinzi wa taarifa binafsi sura ya 44.
Elimu juu ya dhana ya ulinzi wa taarifa binafsi kwa makundi mbalimbali ya kijamii ni endelevu na Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi inatoa elimu hiyo kuwajengea uelewa wahusika wa taarifa binafsi na watumiaji wa taarifa hizo ili uzingatiaji wa ulinzi wa faragha upewe kipaumbele wakati wa kutumia taarifa husika.

WARATIBU NA WASIMAMIZI WA VIHATARI…

DPIA NI LAZIMA, KABLA YA KUANZISHA…

RIDHAA INAPASWA KUTOLEWA BILA SHUR…

TANZANIA DELEGATION PARTICIPATES I…

ROPA NI MUHIMU KWA KILA DPO

𝐓𝐀𝐍𝐙𝐀𝐍𝐈𝐀 𝐀𝐓𝐓𝐄𝐍𝐃𝐄𝐃 𝐓𝐇𝐄 𝐖𝐒𝐈𝐒+𝟐𝟎 𝐇𝐈𝐆𝐇…

DPO SIMAMIA USALAMA WA TAARIFA BIN…

NI LAZIMA KUWA NA SERA YA ULINZI W…

DPIA NI MUHIMU KUIMARISHA ULINZI W…

PDPC KUANZISHA ITHIBATI KWA MAAFIS…

ELIMU YA DHANA YA ULINZI WA TAARIF…

BALOZI ADADI AONGOZA KIKAO CHA BOD…

JENGA UAMINIFU WA TAASISI YAKO KWA…

NI KOSA KUSAMBAZA TAARIFA ZA MTU K…

𝐊𝐔𝐀𝐍𝐃𝐀𝐀 𝐒𝐄𝐑𝐀 𝐘𝐀 𝐔𝐋𝐈𝐍𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐓𝐀𝐀𝐑𝐈𝐅𝐀 …

𝐔𝐒𝐈𝐖𝐄𝐊𝐄 𝐓𝐀𝐀𝐑𝐈𝐅𝐀 𝐙𝐀 𝐌𝐓𝐔 𝐊𝐀𝐌𝐀 𝐌𝐃𝐇𝐀𝐌𝐈…

KUSAFIRISHA TAARIFA BINAFSI NJE YA…

KAMPENI ZIZINGATIE ULINZI WA FARAG…

ULINZI WA FARAGHA KWENYE TAARIFA B…
.
