MISHAHARA KWA WAFANYAKAZI NCHINI KUONGEZEKA JULAI, 2025
May 1, 2025, 8:49 p.m.
Watumishi wa umma nchini Tanzania leo tarehe 01/05/2025 wamepewa habari njema ya kuwepo kwa nyongeza ya mshahara kuanzia mwezi Julai, 2025.
Hayo ameyasema Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan wakati akihutubia kwenye maadhimisho ya siku ya Kimataifa ya wafanyakazi duniani iliyoadhimishwa mkoani Singida Kitaifa hapa Tanzania.
“Ninayofuraha ya kuwatangazia kwamba, katika kuzidi kuleta ustawi kwa wafanyakazi, mwaka huu Serikali itaongeza kima cha chini cha mshahara kwa watumishi wa umma kwa asilimia 35.1. Nyongeza hii itaanza kutumika mwezi Julai 2025 itaongeza kima cha chini cha mshahara kutoka Tsh. 370,000 hadi Tsh. 500,000” amesema Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Pia Mhe. Rais Dkt. Samia ameeleza kuwa Serikali inaendelea kusimamia upatikanaji wa ajira ndani na nje ya Tanzania.
“Jumla ya ajira 8,088,204 zimepatikana kwa kipindi cha Novemba, 2020 hadi Februari, 2025. Ukuaji wa diplomasia ya Tanzania imewezesha ipatikanaji wa fursa za ajira nje ya nchi.”
Hii ni moja ya hatua ambazo serikali inachukua kuwezesha watumishi kustahimili hali ya kiuchumi iliyopo
Maadhimisho hayo ni sehemu ya wafanyakazi kuwasilisha changamoto zao kwa Serikali na kutoa mapendekezo ya nini kifanyike ili kuboresha sekta ya ajira nchini. Kwa mwaka 2025 kauli mbiu yake ni Uchaguzi mkuu 2025 utuletee viongozi wanaojali haki na maslahi ya wafanyakazi, sote tushiriki.

PDPC AND TIRA TO BUILD SUSTAINABLE…

IN DIGITAL ECONOMY PRIVACY SHOULD …

CONTACT US

Mkutano wa Jumuiya ya Afrika Masha…

ULINZI WA TAARIFA BINAFSI UNAANZA …

JAMII YASHAURIWA KULINDA TAARIFA B…

PDPC KUSHIRIKIANA NA WADAU KUIMARI…

PDPC NA HILTON LAW GROUP WAKUTANA …

PDPC TUNAHAKIKISHA ULINZI WA FARAG…

TUZINGATIE KANUNI ZA DHANA YA ULIN…

MSINGI WA UCHUMI WA KIDIJITALI UNA…

‘UNWANTED WITNESS’ WATEMBELEA PDPC

PDPC YASHIRIKI KIKAO - TATHMINI YA…

DKT. MKILIA AFUNGUA WARSHA JUKWAA …

PDPC Yatoa Mafunzo Maalumu kwa Bod…

ELIMU YA DHANA YA ULINZI WA TAARIF…

PDPC YATOA ELIMU KWA UMMA MWANZA

ULINZI WA TAARIFA BINAFSI NI SWALA…

PDPC YATOA WITO WA USAJILI WA TAAS…

MISHAHARA KWA WAFANYAKAZI NCHINI K…