MSINGI WA UCHUMI WA KIDIJITALI UNATEGEMEA ULINZI WA TAARIFA BINAFSI
Feb. 1, 2025, 12:20 a.m.
Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi (PDPC) Dkt. Emmanuel Lameck Mkilia amezungumza katika mkutano wa GovStack, jijini Dar es Salaam na kusisitiza umuhimu wa kulinda faragha wakati mifumo inapoingiliana na kusomana
Mkutano huo uliofanyika kwa siku mbili na kufikia tamati leo uliandaliwa na Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari kwa kushirikiana na jitihada ya GovStack kutoka nchini Estonia na uliangazia mifumo ya afya ya kidigitali, ambapo Dkt. Mkilia ameelezea majukumu ya PDPC katika kuhakikisha faragha inazingatiwa, hasa katika nyanja za afya katika dunia ya kidijitali.
Aidha, Dkt. Mkilia alitaja hatua zinazochukuliwa ili kulinda taarifa binafsi za kiafya na umuhimu wa kuaminika ili watu waweze kushiriki kikamilifu katika uchumi wa kidijitali bila hofu.
“Msingi wa uchumi huu wa kidijitali unategemea ulinzi wa taarifa binafsi na faragha.” Amesema Dkt. Mkilia
Mkutano huo ulihudhuriwa na wajumbe kutoka Wizara ya Afya, Ofisi ya Rais TAMISEMI, hospitali za serikali na binafsi kutoka Tanzania bara na Zanzibar.

PDPC AND TIRA TO BUILD SUSTAINABLE…

IN DIGITAL ECONOMY PRIVACY SHOULD …

CONTACT US

Mkutano wa Jumuiya ya Afrika Masha…

ULINZI WA TAARIFA BINAFSI UNAANZA …

JAMII YASHAURIWA KULINDA TAARIFA B…

PDPC KUSHIRIKIANA NA WADAU KUIMARI…

PDPC NA HILTON LAW GROUP WAKUTANA …

PDPC TUNAHAKIKISHA ULINZI WA FARAG…

TUZINGATIE KANUNI ZA DHANA YA ULIN…

KIKAO KAMATI YA BUNGE YA MIUNDOMBI…

MSINGI WA UCHUMI WA KIDIJITALI UNA…

‘UNWANTED WITNESS’ WATEMBELEA PDPC

PDPC YASHIRIKI KIKAO - TATHMINI YA…

DKT. MKILIA AFUNGUA WARSHA JUKWAA …

PDPC Yatoa Mafunzo Maalumu kwa Bod…

ELIMU YA DHANA YA ULINZI WA TAARIF…

PDPC YATOA ELIMU KWA UMMA MWANZA

ULINZI WA TAARIFA BINAFSI NI SWALA…