RIDHAA INAPASWA KUTOLEWA BILA SHURUTI
June 24, 2025, 2 p.m.
Wakusanyaji na wachakataji wa Taarifa Nchini wameshauriwa kukusanya na kuchakata Taarifa kwa kuzingatia matakwa ya Sheria ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi Sura ya 44 (PDPA) ikiwa ni pamoja na kutowashurutisha wahusika wa Taarifa kuwapatia ridhaa.
Wito huo umetolewa jijini Arusha, leo Juni 24, 2025 na Wakili Humphrey Mtuy, Mkuu wa Kitengo cha Sheria,Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi (PDPC). Wakati akitoa mada ya Masuala Muhimu ya Kisheria katika PDPA kwa washiriki wa mafunzo ya kupunguza madhara ya vihatarishi katika Ulinzi wa Taarifa Binafsi ambapo amesema kwa mujibu wa PDPA hairuhisiwi kuchukua ridhaa ya Muhusika wa Taarifa kwa Shuruti.
“Sheria ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi Kifungu cha Thelathini (30) kifungu kidogo cha Kwanza (1) na Kanuni ya Ishirini na Tano 25 (d) ya Ukusanyaji na Uchakataji wa Taarifa imeanisha mazingira ya kuchukua ridhaa kwa Muhusika wa Taarifa hivyo inapaswa kutoa ridhaa bila shuruti” Amesema Wakili Mtuy
Aidha wakili Mtuy alikamilisha mada yake kwa kusema kwamba PDPA imekuja kumlinda muhusika wa Taarifa na imeruhusu PDPC kushirikiana na vyombo vingine vya dola kumpatia haki ya Faragha Muhusika wa Taarifa endapo Taarifa zake zikitumika vibaya.

PDPC TUNAHAKIKISHA ULINZI WA FARAG…

MSINGI WA UCHUMI WA KIDIJITALI UNA…

‘UNWANTED WITNESS’ WATEMBELEA PDPC

PDPC YASHIRIKI KIKAO - TATHMINI YA…

DKT. MKILIA AFUNGUA WARSHA JUKWAA …

PDPC Yatoa Mafunzo Maalumu kwa Bod…

ELIMU YA DHANA YA ULINZI WA TAARIF…

PDPC YATOA ELIMU KWA UMMA MWANZA

ULINZI WA TAARIFA BINAFSI NI SWALA…

PDPC YATOA WITO WA USAJILI WA TAAS…

MISHAHARA KWA WAFANYAKAZI NCHINI K…

PDPC YATANGAZA MAFUNZO KWA MAAFISA…

SIMAMIENI MIPANGO YA KUPUNGUZA VIH…

RISK CHAMPIONS NA DPO’s SHIRIKIANE…

WARATIBU NA WASIMAMIZI WA VIHATARI…

DPIA NI LAZIMA, KABLA YA KUANZISHA…

RIDHAA INAPASWA KUTOLEWA BILA SHUR…

TANZANIA DELEGATION PARTICIPATES I…