ULINZI WA FARAGHA KWENYE TAARIFA BINAFSI UNAJENGA IMANI YA WANANCHI KWA TAASISI
Sept. 11, 2025, 11:23 a.m.
Mkurugenzi wa Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi Ofisi ya Zanzibar Bi. Rehema Abdalla ameukumbusha Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa watumishi wa Umma (PSSSF) kuendelea kutunza faragha za taarifa za wateja wao kwa kuhakikisha wanatumia taarifa wanazozikusanya au kuzichakata kwa misingi inayokusudiwa tu.
Bi. Rehema ameyasema hayo katika mafunzo ya siku moja kwa watumishi wa Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi Ofisi ya Zanzibar yaliyotolea na Afisa wa PSSSF Bw. Seif Khamis yakilenga kuwajengea uelewa watumishi hao juu ya utekelezaji wa shughuli za Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa watumishi wa Umma.
“Ninausifu Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa watumishi wa Umma kwa kutumia teknolojia mpya inayorahisisha upatikanaji wa huduma kwa wateja. Nawasihi katika utekelezaji wa shughuli zenu kuzingatia faragha katika kukusanya na kuchakata taarifa za wateja wenu ili kujenga imani kwa wanachama wa mfuko huo” amesema Bi. Rehema
Msisitizo wa ulinzi wa faragha za taarifa za watu ni njia mojawapo ya kuunga mkono juhudi za Serikali kupitia Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi kuhakikisha taasisi zote za umma na binafsi zinazingatia kanuni za ulinzi wa faragha, ili kujenga imani ya wananchi katika mifumo ya kidigitali.

WARATIBU NA WASIMAMIZI WA VIHATARI…

DPIA NI LAZIMA, KABLA YA KUANZISHA…

RIDHAA INAPASWA KUTOLEWA BILA SHUR…

TANZANIA DELEGATION PARTICIPATES I…

ROPA NI MUHIMU KWA KILA DPO

𝐓𝐀𝐍𝐙𝐀𝐍𝐈𝐀 𝐀𝐓𝐓𝐄𝐍𝐃𝐄𝐃 𝐓𝐇𝐄 𝐖𝐒𝐈𝐒+𝟐𝟎 𝐇𝐈𝐆𝐇…

DPO SIMAMIA USALAMA WA TAARIFA BIN…

NI LAZIMA KUWA NA SERA YA ULINZI W…

DPIA NI MUHIMU KUIMARISHA ULINZI W…

PDPC KUANZISHA ITHIBATI KWA MAAFIS…

ELIMU YA DHANA YA ULINZI WA TAARIF…

BALOZI ADADI AONGOZA KIKAO CHA BOD…

JENGA UAMINIFU WA TAASISI YAKO KWA…

NI KOSA KUSAMBAZA TAARIFA ZA MTU K…

𝐊𝐔𝐀𝐍𝐃𝐀𝐀 𝐒𝐄𝐑𝐀 𝐘𝐀 𝐔𝐋𝐈𝐍𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐓𝐀𝐀𝐑𝐈𝐅𝐀 …

𝐔𝐒𝐈𝐖𝐄𝐊𝐄 𝐓𝐀𝐀𝐑𝐈𝐅𝐀 𝐙𝐀 𝐌𝐓𝐔 𝐊𝐀𝐌𝐀 𝐌𝐃𝐇𝐀𝐌𝐈…

KUSAFIRISHA TAARIFA BINAFSI NJE YA…

KAMPENI ZIZINGATIE ULINZI WA FARAG…

ULINZI WA FARAGHA KWENYE TAARIFA B…
.
