π”π’πˆπ–π„πŠπ„ π“π€π€π‘πˆπ…π€ 𝐙𝐀 πŒπ“π” πŠπ€πŒπ€ πŒπƒπ‡π€πŒπˆππˆ π–π€πŠπŽ ππˆπ‹π€ πŠπ”ππ€π“π€ π‘πˆπƒπ‡π€π€ π˜π€πŠπ„

Aug. 21, 2025, 2:46 p.m. π”π’πˆπ–π„πŠπ„ π“π€π€π‘πˆπ…π€ 𝐙𝐀 πŒπ“π” πŠπ€πŒπ€ πŒπƒπ‡π€πŒπˆππˆ π–π€πŠπŽ ππˆπ‹π€ πŠπ”ππ€π“π€ π‘πˆπƒπ‡π€π€ π˜π€πŠπ„

Ni kosa kisheria kuweka Taarifa za mtu kama mdhamini wako bila kupata ridhaa yake.

Haya yamesemwa leo Agosti 21,2025 na Mkurugenzi wa Usajili na Uzingatiaji wa Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi (PDPC), Mhandisi Stephen Wangwe Β wakati akijibu maswali mbalimbali kutoka kwa Washiriki wa Mafunzo Maalumu ya Maafisa Ulinzi wa Taarifa (DPOs) yanayoendelea hapa mjini Morogoro.Β 

Mhandisi wangwe amesema kwa mujibu wa Sheria ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi, Sura ya 44 (PDPA) ni kosa kutumia taarifa yoyote ya mtu bila ridhaa yake. Hivyo hata wale wanaoweka taarifa za watu kama wadhamini wao bila kupata ridhaa wanaenda kinyume na Sheria.

"Kuna baadhi wa watu kwenye jamii wanaandika taarifa za wadhamini sehemu mbalimbali bila kuomba ridhaa za wahusika. Mfano kwenye barua za maombi ya kazi au kwenye maombi ya mkopo, hii ni kinyume na sheria na haipaswi kuwa hivyo" Amesema Mhandisi WangweΒ 

Akijibu swali lingine kuhusu baadhi ya watafiti wanaokusanya na kuchakata taarifa nyeti za watu bila kupata ridhaa, Mhandisi wangwe amesema wakusanyaji na wachakataji wa taarifa wanapokua kwenye majukumu yao ya kikazi wanapaswa kuzingatia haki za muhusika wa taarifa Β kwakua PDPA ipo kumlinda muhusika wa taarifa.

Zaidi ya DPO's 200 kutoka ndani na nje ya nchi wameshiriki kwenye awamu hii ya nne ya mafunzo maalumu ya Maafisa Ulinzi wa Taarifa ambayo yameanza Agosti 20 na yatafikia tamati Agosti 22, 2025.

SIMAMIENI MIPANGO YA KUPUNGUZA VIHATARISHI KWENYE ULINZI WA TAARIFA BINAFSI

SIMAMIENI MIPANGO YA KUPUNGUZA VIH…

June 23, 2025, 7:05 p.m.
RISK CHAMPIONS NA DPO’s SHIRIKIANENI KULINDA TAARIFA BINAFSI NCHINI

RISK CHAMPIONS NA DPO’s SHIRIKIANE…

June 23, 2025, 7:18 p.m.
WARATIBU NA WASIMAMIZI WA VIHATARISHI NCHINI TIMIZENI WAJIBU WENU

WARATIBU NA WASIMAMIZI WA VIHATARI…

June 23, 2025, 6:28 p.m.
DPIA NI LAZIMA, KABLA YA KUANZISHA MRADI UNAOKUSANYA NA KUCHAKATA …

DPIA NI LAZIMA, KABLA YA KUANZISHA…

June 23, 2025, 8 p.m.
RIDHAA INAPASWA KUTOLEWA BILA SHURUTI

RIDHAA INAPASWA KUTOLEWA BILA SHUR…

June 24, 2025, 2 p.m.
TANZANIA DELEGATION PARTICIPATES IN UN CSTD MULTI-STAKEHOLDERS WORKING GROUP ON …

TANZANIA DELEGATION PARTICIPATES I…

July 4, 2025, 8 a.m.
ROPA NI MUHIMU KWA KILA DPO

ROPA NI MUHIMU KWA KILA DPO

July 2, 2025, 3:55 p.m.
π“π€ππ™π€ππˆπ€ 𝐀𝐓𝐓𝐄𝐍𝐃𝐄𝐃 𝐓𝐇𝐄 π–π’πˆπ’+𝟐𝟎 π‡πˆπ†π‡-𝐋𝐄𝐕𝐄𝐋 𝐄𝐕𝐄𝐍𝐓 𝐈𝐍 𝐆𝐄𝐍𝐄𝐕𝐀

π“π€ππ™π€ππˆπ€ 𝐀𝐓𝐓𝐄𝐍𝐃𝐄𝐃 𝐓𝐇𝐄 π–π’πˆπ’+𝟐𝟎 π‡πˆπ†π‡β€¦

July 7, 2025, 9:05 a.m.
DPO SIMAMIA USALAMA WA TAARIFA BINAFSI KWENYE TAASISI/KAMPUNI YAKO

DPO SIMAMIA USALAMA WA TAARIFA BIN…

July 9, 2025, 5:26 p.m.
NI LAZIMA KUWA NA SERA YA ULINZI WA TAARIFA KWENYE …

NI LAZIMA KUWA NA SERA YA ULINZI W…

July 10, 2025, 3:54 p.m.
DPIA NI MUHIMU KUIMARISHA ULINZI WA TAARIFA BINAFSI

DPIA NI MUHIMU KUIMARISHA ULINZI W…

July 11, 2025, 3:55 p.m.
PDPC KUANZISHA ITHIBATI KWA MAAFISA ULINZI WA TAARIFA BINAFSI NCHINI

PDPC KUANZISHA ITHIBATI KWA MAAFIS…

July 16, 2025, 3:07 p.m.
ELIMU YA DHANA YA ULINZI WA TAARIFA BINAFSI YATOLEWA MAONESHO …

ELIMU YA DHANA YA ULINZI WA TAARIF…

Aug. 10, 2025, 4:24 p.m.
BALOZI ADADI AONGOZA KIKAO CHA BODI YA WAKURUGENZI PDPC

BALOZI ADADI AONGOZA KIKAO CHA BOD…

Aug. 14, 2025, 3:55 p.m.
JENGA UAMINIFU WA TAASISI YAKO KWA WADAU KWA KULINDA TAARIFA …

JENGA UAMINIFU WA TAASISI YAKO KWA…

Aug. 20, 2025, 8:57 p.m.
NI KOSA KUSAMBAZA TAARIFA ZA MTU KWENYE MITANDAO YA KIJAMII …

NI KOSA KUSAMBAZA TAARIFA ZA MTU K…

Aug. 20, 2025, 8:58 p.m.
πŠπ”π€ππƒπ€π€ 𝐒𝐄𝐑𝐀 π˜π€ π”π‹πˆππ™πˆ 𝐖𝐀 π“π€π€π‘πˆπ…π€ ππˆππ€π…π’πˆ πŠπ–π„ππ˜π„ π“π€π€π’πˆπ’πˆ 𝐍𝐈 …

πŠπ”π€ππƒπ€π€ 𝐒𝐄𝐑𝐀 π˜π€ π”π‹πˆππ™πˆ 𝐖𝐀 π“π€π€π‘πˆπ…π€ …

Aug. 21, 2025, 2:38 p.m.
π”π’πˆπ–π„πŠπ„ π“π€π€π‘πˆπ…π€ 𝐙𝐀 πŒπ“π” πŠπ€πŒπ€ πŒπƒπ‡π€πŒπˆππˆ π–π€πŠπŽ ππˆπ‹π€ πŠπ”ππ€π“π€ π‘πˆπƒπ‡π€π€ …

π”π’πˆπ–π„πŠπ„ π“π€π€π‘πˆπ…π€ 𝐙𝐀 πŒπ“π” πŠπ€πŒπ€ πŒπƒπ‡π€πŒπˆβ€¦

Aug. 21, 2025, 2:46 p.m.
KUSAFIRISHA TAARIFA BINAFSI NJE YA NCHI NI LAZIMA KUPATA KIBALI …

KUSAFIRISHA TAARIFA BINAFSI NJE YA…

Aug. 22, 2025, 4:45 p.m.
Tanzania Census 2022