KAMPENI ZIZINGATIE ULINZI WA FARAGHA KWENYE TAARIFA BINAFSI ZA WATU
Sept. 5, 2025, 8:56 a.m.
Mkurugenzi Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi Ofisi ya Zanzibar, Bi Rehema Abdalla amewataka wagombea wa ngazi zote nchini kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 kuhakikisha hawaingilii faragha za watu.
Bi. Rehema amezungumza hayo wakati akifanya mahojiano maalum na mtangazaji Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) Bi. Nasra Khatib kuhusu umuhimu wa kulinda taarifa binafsi katika kampeni za uchaguzi mkuu kwa wagombea watakaonadi sera za vyama vyao.
βWagombea wa ngazi zote hakikisheni hamuingilii faragha za watu na majukwaa mnayotumia kunadi sera za vyama vyenu yasitumike kukiuka misingi ya Sheria ya Ulinzi wa taarifa binafsiβ amesema Bi. Rehema.
Akisisitiza swala hili, Bi. Rehema amesema kuwa kuchapisha taarifa binafsi za mtu kwenye magazeti, mitandao ya kijamii au kutangaza kwenye redio na televisheni bila ridhaa ya muhusika wa taarifa hizo ni kinyume na matakwa ya Sheria ya Ulinzi wa taarifa binafsi sura ya 44.
Elimu juu ya dhana ya ulinzi wa taarifa binafsi kwa makundi mbalimbali ya kijamii ni endelevu na Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi inatoa elimu hiyo kuwajengea uelewa wahusika wa taarifa binafsi na watumiaji wa taarifa hizo ili uzingatiaji wa ulinzi wa faragha upewe kipaumbele wakati wa kutumia taarifa husika.
ROPA NI MUHIMU KWA KILA DPO
ππππππππ ππππππππ πππ ππππ+ππ ππππβ¦
DPO SIMAMIA USALAMA WA TAARIFA BINβ¦
NI LAZIMA KUWA NA SERA YA ULINZI Wβ¦
DPIA NI MUHIMU KUIMARISHA ULINZI Wβ¦
PDPC KUANZISHA ITHIBATI KWA MAAFISβ¦
ELIMU YA DHANA YA ULINZI WA TAARIFβ¦
BALOZI ADADI AONGOZA KIKAO CHA BODβ¦
JENGA UAMINIFU WA TAASISI YAKO KWAβ¦
NI KOSA KUSAMBAZA TAARIFA ZA MTU Kβ¦
πππππππ ππππ ππ ππππππ ππ ππππππ π β¦
πππππππ ππππππ π ππ πππ ππππ ππππππβ¦
KUSAFIRISHA TAARIFA BINAFSI NJE YAβ¦
KAMPENI ZIZINGATIE ULINZI WA FARAGβ¦
ULINZI WA FARAGHA KWENYE TAARIFA Bβ¦
PDPC na NHIF Kuimarisha Ushirikianβ¦
ELIMU YA KUZUIA NA KUPAMBANA NA RUβ¦
DPOs WAIPONGEZA PDPC KWA KUWAJENGEβ¦
KARIBU PDPC MHE. ANGELLAH JASMINE β¦
KIKAO CHA SABA CHA BODI YA WAKURUGβ¦