NI KOSA KUSAMBAZA TAARIFA ZA MTU KWENYE MITANDAO YA KIJAMII BILA RIDHAA YAKE

Aug. 20, 2025, 9:04 p.m. NI KOSA KUSAMBAZA TAARIFA ZA MTU KWENYE MITANDAO YA KIJAMII BILA RIDHAA YAKE

Jamii yakumbushwa kutokusambaza au kutumia taarifa za mtu bila ridhaa ya mwenye taarifa.

Ushauri huo wa kisheria umetolewa leo Agosti 20, 2025 na Wakili Godfrey Assenga, Mwanasheria wa Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi (PDPC) wakati akijibu swali la mmoja wa washiriki wa Mafunzo Maalumu ya Maafisa Ulinzi wa Taarifa (DPO's) yanayoendelea hapa Morena Hoteli Mkoani Morogoro, ambapo aliulizwa je wale wanaosamba taarifa za watu kwenye makundi sogozi (WhatsApp groups) bila kuwa na ridhaa ya wahusika wa taarifa hizo nao wanavunja Sheria ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi, Sura ya 44 (PDPA)?

Akijibu swali hilo Wakili Asenga amesema, ndio ni kosa kisheria kwa mujibu wa Kanuni za Ukusanyaji na Uchakataji wa Taarifa Binafsi za mwaka 2023 na akasisitiza hata wale wanaosamba taarifa za watu kupitia mitandao ya kijamii hawaruhusiwi kufanya hivyo kama hawajapata ridhaa ya muhusika wa taarifa.

"Kanuni ya 15 (1) ya Kanuni za ukusanyaji na uchakataji wa taarifa binafsi za mwaka 2023 inazungumza mhusika wa taarifa anaweza kuomba kwa mkusanyaji au mchakataji kusitisha ukusanyaji au uchakataji wa taarifa binafsi muda wowote hivyo muhusika wa taarifa akiomba ridhaa ya kufutwa kwa taarifa zake unapaswa kumsikiliza na kuzifuta na endapo ukikaidi ombi lake ana haki ya kuja kulalamika PDPC na Sheria itafata mkondo wake” Amesema Wakili Asenga

Aidha Wakili Asenga alihitimisha kujibu swali hilo kwa kunukuu msemo maarufu wa kutokujua Sheria sio kigezo cha kuvunja Sheria.

ROPA NI MUHIMU KWA KILA DPO

ROPA NI MUHIMU KWA KILA DPO

July 2, 2025, 3:55 p.m.
π“π€ππ™π€ππˆπ€ 𝐀𝐓𝐓𝐄𝐍𝐃𝐄𝐃 𝐓𝐇𝐄 π–π’πˆπ’+𝟐𝟎 π‡πˆπ†π‡-𝐋𝐄𝐕𝐄𝐋 𝐄𝐕𝐄𝐍𝐓 𝐈𝐍 𝐆𝐄𝐍𝐄𝐕𝐀

π“π€ππ™π€ππˆπ€ 𝐀𝐓𝐓𝐄𝐍𝐃𝐄𝐃 𝐓𝐇𝐄 π–π’πˆπ’+𝟐𝟎 π‡πˆπ†π‡β€¦

July 7, 2025, 9:05 a.m.
DPO SIMAMIA USALAMA WA TAARIFA BINAFSI KWENYE TAASISI/KAMPUNI YAKO

DPO SIMAMIA USALAMA WA TAARIFA BIN…

July 9, 2025, 5:26 p.m.
NI LAZIMA KUWA NA SERA YA ULINZI WA TAARIFA KWENYE …

NI LAZIMA KUWA NA SERA YA ULINZI W…

July 10, 2025, 3:54 p.m.
DPIA NI MUHIMU KUIMARISHA ULINZI WA TAARIFA BINAFSI

DPIA NI MUHIMU KUIMARISHA ULINZI W…

July 11, 2025, 3:55 p.m.
PDPC KUANZISHA ITHIBATI KWA MAAFISA ULINZI WA TAARIFA BINAFSI NCHINI

PDPC KUANZISHA ITHIBATI KWA MAAFIS…

July 16, 2025, 3:07 p.m.
ELIMU YA DHANA YA ULINZI WA TAARIFA BINAFSI YATOLEWA MAONESHO …

ELIMU YA DHANA YA ULINZI WA TAARIF…

Aug. 10, 2025, 4:24 p.m.
BALOZI ADADI AONGOZA KIKAO CHA BODI YA WAKURUGENZI PDPC

BALOZI ADADI AONGOZA KIKAO CHA BOD…

Aug. 14, 2025, 3:55 p.m.
JENGA UAMINIFU WA TAASISI YAKO KWA WADAU KWA KULINDA TAARIFA …

JENGA UAMINIFU WA TAASISI YAKO KWA…

Aug. 20, 2025, 8:57 p.m.
NI KOSA KUSAMBAZA TAARIFA ZA MTU KWENYE MITANDAO YA KIJAMII …

NI KOSA KUSAMBAZA TAARIFA ZA MTU K…

Aug. 20, 2025, 8:58 p.m.
πŠπ”π€ππƒπ€π€ 𝐒𝐄𝐑𝐀 π˜π€ π”π‹πˆππ™πˆ 𝐖𝐀 π“π€π€π‘πˆπ…π€ ππˆππ€π…π’πˆ πŠπ–π„ππ˜π„ π“π€π€π’πˆπ’πˆ 𝐍𝐈 …

πŠπ”π€ππƒπ€π€ 𝐒𝐄𝐑𝐀 π˜π€ π”π‹πˆππ™πˆ 𝐖𝐀 π“π€π€π‘πˆπ…π€ …

Aug. 21, 2025, 2:38 p.m.
π”π’πˆπ–π„πŠπ„ π“π€π€π‘πˆπ…π€ 𝐙𝐀 πŒπ“π” πŠπ€πŒπ€ πŒπƒπ‡π€πŒπˆππˆ π–π€πŠπŽ ππˆπ‹π€ πŠπ”ππ€π“π€ π‘πˆπƒπ‡π€π€ …

π”π’πˆπ–π„πŠπ„ π“π€π€π‘πˆπ…π€ 𝐙𝐀 πŒπ“π” πŠπ€πŒπ€ πŒπƒπ‡π€πŒπˆβ€¦

Aug. 21, 2025, 2:46 p.m.
KUSAFIRISHA TAARIFA BINAFSI NJE YA NCHI NI LAZIMA KUPATA KIBALI …

KUSAFIRISHA TAARIFA BINAFSI NJE YA…

Aug. 22, 2025, 4:45 p.m.
KAMPENI ZIZINGATIE ULINZI WA FARAGHA KWENYE TAARIFA BINAFSI ZA WATU

KAMPENI ZIZINGATIE ULINZI WA FARAG…

Sept. 5, 2025, 8:53 a.m.
ULINZI WA FARAGHA KWENYE TAARIFA BINAFSI UNAJENGA IMANI YA WANANCHI …

ULINZI WA FARAGHA KWENYE TAARIFA B…

Sept. 11, 2025, 11:23 a.m.
PDPC na NHIF Kuimarisha Ushirikiano katika Kulinda Faragha na Taarifa …

PDPC na NHIF Kuimarisha Ushirikian…

Nov. 12, 2025, 6:56 p.m.
ELIMU YA KUZUIA NA KUPAMBANA NA RUSHWA YAWAFIKIA PDPC

ELIMU YA KUZUIA NA KUPAMBANA NA RU…

Nov. 24, 2025, 10:12 p.m.
DPOs WAIPONGEZA PDPC KWA KUWAJENGEA UWEZO KATIKA ULINZI WA TAARIFA

DPOs WAIPONGEZA PDPC KWA KUWAJENGE…

Dec. 4, 2025, 7:08 p.m.
KARIBU PDPC MHE. ANGELLAH JASMINE MBELWA KAIRUKI

KARIBU PDPC MHE. ANGELLAH JASMINE …

Dec. 15, 2025, 7 p.m.
KIKAO CHA SABA CHA BODI YA WAKURUGENZI PDPC

KIKAO CHA SABA CHA BODI YA WAKURUG…

Dec. 19, 2025, 11:50 p.m.