PDPC KUANZISHA ITHIBATI KWA MAAFISA ULINZI WA TAARIFA BINAFSI NCHINI
July 16, 2025, 3:10 p.m.
Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi (PDPC) ipo katika mpango wa kuwa na Ithibati kwa Maafisa Ulinzi wa Taarifa (DPOs) ili kuhakikisha ulinzi wa taarifa binafsi nchini unazingatiwa.
Hatua hii inalenga kuimarisha ulinzi wa taarifa binafsi na kuhakikisha kuwa waliopewa jukumu la ulinzi wa faragha za taarifa hizo wanazingatia viwango vya juu vya ufanisi na uadilifu.
Hayo yamesemwa leo tarehe 16/07/2025 na Mkurugenzi Mkuu wa PDPC Dkt. Emmanuel Mkilia alipotembelea kituo cha mafunzo maalum ya maafisa ulinzi wa taarifa kilichopo kwenye hoteli ya Morena, Morogoro na kuzungumza na washiriki wa mafunzo hayo ambapo alisisitiza kuwa mafunzo hayo ni hatua muhimu ya kuleta mazingira rafiki na yenye ufanisi kati ya PDPC na DPOs.
“Tunatarajia kuanzisha mfumo wa mafunzo utakaoakisi uthibitisho wa kitaalamu wa DPOs. Hii inamaanisha kwamba, bila cheti rasmi cha utambuzi wako kutoka PDPC, huwezi kuwa DPO halali,” alisisitiza Dkt. Mkilia.
Hii ni hatua madhubuti inayolenga kuimarisha ulinzi wa taarifa binafsi, kuhakikisha maafisa wanaotekeleza majukumu haya wanazingatia viwango vya kitaifa na kimataifa, na kuleta ufanisi wa kiutendaji katika sekta hiyo muhimu kwa ulinzi wa faragha kwenye taarifa binafsi za watu na mashirika nchini.

DKT. MKILIA AFUNGUA WARSHA JUKWAA …

PDPC Yatoa Mafunzo Maalumu kwa Bod…

ELIMU YA DHANA YA ULINZI WA TAARIF…

PDPC YATOA ELIMU KWA UMMA MWANZA

ULINZI WA TAARIFA BINAFSI NI SWALA…

PDPC YATOA WITO WA USAJILI WA TAAS…

MISHAHARA KWA WAFANYAKAZI NCHINI K…

PDPC YATANGAZA MAFUNZO KWA MAAFISA…

SIMAMIENI MIPANGO YA KUPUNGUZA VIH…

RISK CHAMPIONS NA DPO’s SHIRIKIANE…

WARATIBU NA WASIMAMIZI WA VIHATARI…

DPIA NI LAZIMA, KABLA YA KUANZISHA…

RIDHAA INAPASWA KUTOLEWA BILA SHUR…

TANZANIA DELEGATION PARTICIPATES I…

ROPA NI MUHIMU KWA KILA DPO

𝐓𝐀𝐍𝐙𝐀𝐍𝐈𝐀 𝐀𝐓𝐓𝐄𝐍𝐃𝐄𝐃 𝐓𝐇𝐄 𝐖𝐒𝐈𝐒+𝟐𝟎 𝐇𝐈𝐆𝐇…

DPO SIMAMIA USALAMA WA TAARIFA BIN…

NI LAZIMA KUWA NA SERA YA ULINZI W…

DPIA NI MUHIMU KUIMARISHA ULINZI W…

PDPC KUANZISHA ITHIBATI KWA MAAFIS…